Mwenyekiti  wa  Idara  ya  Misioni  ya  Esarkia ya Kipatriarki ya Afrika, Padri Georgi Maksimov, azuru Kamerun - Esarkia ya Kipatriarki ya Afrika
RUS | ENG | FRA | SWA | DEU | عرب | Ελλ | PT

Mwenyekiti  wa  Idara  ya  Misioni  ya  Esarkia ya Kipatriarki ya Afrika, Padri Georgi Maksimov, azuru Kamerun

Ziara ilianza kwa kufanya mkutano wa kichungaji na makasisi wa kanisa la Esarkia nchini Kameruni. Washiriki walijadili mipango ya maendeleo ya utume nchini humo,wakatatua masuala kadhaa ya kiutawala  pamoja  na changamoto zinazoikabili parokia.

Tarehe 12 Februari 2023, katika Wiki ya Mwana Mpotevu, siku ya kumbukizi ya walimu wa kiekumeni  na watakatifu  Basil Mkuu, Gregori  Mtheolojia na  Yohana Zlatousti,  iliadhimishwa  Liturgia  ya upatanisho katika kanisa  la Ufufuo wa Kristo mjini Yaunde –  mji mkuu wa Kameruni. Ibada  takatifu  iliongozwa na Padri  Georgi, huku makasisi wa Esarkia wakihudumu pamoja naye.

Katika  kuhitimisha la ibada, Padri Georgi alitunuku  vyeti  vya  heshima kwa waumini  vijana – washindi wa shindano la Mchoro wa Uothodoksi  na  akawapa tuzo za ukumbusho.

Siku hiyo hiyo, Baba Padri Georgi alikutana na “askofu” wa kikundi kisicho na uhalali  kisheria, akitaka kujiunga na Kanisa la Kiothodoksi la Urusi. Kwa mujibu wa taratibu, kuhamia  kwake  kunawezekana  endapo tu atakuja kama mtu  wa kawaida.

Aidha, mara kadhaa kumepokelewa maombi ya makasisi wa Metropolia ya Kameruni ya Kanisa la Aleksandria, wakitaka  kuhamia Patriarkia  ya Mosko, na yanafikiriwa.

Shirikisha katika mitandao ya kijamii:

Taarifa zote zilizo na maneno muhimu

-